Wednesday, 22 May 2013

MAKALA : IJUE HISTORIA YA ASKOFU MOSES KULOLA AMBAYE ANAONGOZA MAKANISA 4000


Moses Kulola, alizaliwa mwezi Juni 1928, katika familia ya watoto kumi, na watano kati yao bado ni hai. alisajiliwa katika shule ya kwanza mwaka 1939 iitwayo Ligsha Sukuma shule ya misheni baada ya Ligsha, alijiunga na taasisi ya usanifu mwaka 1949. Alibatizwa mwaka 1950 katika Kanisa la AIC Makongoro.
Ni mume wa Elizabeth na wamezaa watoto10 ambapo saba bado hai.alianza kazi za kimisionari mwaka1950 japokuwa aliitwa mwaka 1949 mara tu baada ya kubatizwa.

Mwaka 1959 alianza kufanya kazi serikalini, wakati huo huo akihubiri Injili katika miji na vijiji. Utumishi wake mkubwa kwa nchi ulifika mwisho mwaka 1962, ambapo aliamua kujitolea moja kwa moja nguvu zake zote, mwili na nafsi. Mwaka 1964 alijiunga na chuo cha kiteolojia na 1966 alitunukiwa stashahada.


Hakuacha elimu pale tu, aliendelea na masomo mbalimbali ambapo alitunukiwa vyeti mbalimbali katika mataifa mbalimbali.


Alihudumu kikazi kwa miaka miwili kama Mchungaji kabla ya kuwa mpentekoste mnamo 1961-1962, alifanya kazi katika kanisa la TAG 1966 mpaka 1991 ambapo aliamua kuanzishaa makanisa Evangelistic Assemblies God (EAGT), ambapo yalifanikiwa kukua kwa kasi kubwa katika nchi za Tanzania, Zambia , Malawi na kwa ujumla kuna makanisa yapatayo 4000 katika nchi mbalimbali yakiwemo makubwa na madogo
Askofu Moses Kulola anayeongoza makanisa elfu nne, Askofu Msaidizi wake ni Mwaisabila.

Askofu Kulola aliyeketi akiwa na waimbaji wa injili nchini Mwinjilisti Faustin Munishi mkono wa kushoto pamoja na Emmanuel Mwasota. mwanzoni mwa mwaka 1970
Mchakato wa kuongoza makanisa elfu nne si rahisi na kwamba kumefanyika mgawanyiko wa majimbo yasiyopungua 34 ya kazi na kanda tano kwa ajili ya kurahisisha kazi na kila kanda na jimbo lina mwangalizi wake. Nampenda sana Askofu Moses Kulola maana anafanya kazi ya MUNGU kwa moyo na kwa mujibu wa kitabu cha historia yake Askofu Kulola amezunguka Tanzania nzima tena wakati mwingine kwa kutembea kwa miguu na kwenye mazingira magumu sana kiasi kwamba ni wito mkuu wa MUNGU mkuu alionao Askofu Kulola na kwa miaka zaidi ya 60 amekuwa akihubiri neno la MUNGU na hadi sasa MUNGU anamtumia sana, katika mkutano uliopita wa askofu Kulola pale viwanja vya jangwani jijini Dar es salaam maelfu ya watu walihudhulia na wengi sana kufunguliwa na injili anayohubiri askofu Kulola ni injili iliyonyooka na akiwataka wanadamu kumpa YESU KRISTO maisha yao ili wapate uzima wa milele bure.

Tuesday, 21 May 2013

MAMBO HAYAJILETI YENYEWE - MAMBO YANASABABISHWA KUTOKEA.


Na Mwalimu Alfred Katuma.

5 Naam ,na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu,
Katika imani yenu tieni na wema na katia wema wenu maarifa……….”.
(1pet.1:5)
Bwana akufunulie akili zako ili uelewe hiki tunachojifunza lakini pia akusaidie kuyaweka kwenye matendo haya unayojifunza. Sasa hivi tunaishi kwenye nyakati ambazo kumezuka mafundisho yenye msisitizo mkubwa sana kwenye upande mmoja wa miujiza kiasi kwamba watu wengi sana wamejikuta wanaishi maisha ya kimiujiza miujiza,naamanisha watu wamekuwa wanaishi wakitegemea kufanikiwa katika maisha kwa miujiza tu unakuta mtu hataki kufanya kazi anategemea akienda kuwekewa mikono na watumishi basi mambo yatajileta yenyewe tu! Kwa sababu ya watu wengi kutaka kuishi kimiujiza wamejikuta kila kitu wanaita muujiza, unakuta mtu kafanikiwa kununua gari eti anaita muujiza au mtu kwenda ulaya anaita muujiza, mama kanunuliwa kanga na mumewe anaita muujiza. 

Sijui kwa nini nimeanza kwa style hii lakini ninamini kuna kitu Mungu anataka tujifunze hapa na nianze kuelezea  kuhusu muujiza. Ukisoma katika kamusi ya Kiswahili sanifu inafafanua neno muujiza kama jambo lisilokuwa la kawaida. Kwa maana  nyingine muujiza ni matendo yanayofanyika kinyume na maumbile ya asili ni mambo ambayo hata ukimwambia mwanasayansi afafanue hawezi kuyafafanua yametokeaje, lakini utakuta mtumishi wa  Mungu anamuombea mtu anasema ,”pokea muujiza wa kwenda ulaya! Pokea muujiza wa gari pokea muujiza wa nyumba! Na maombi mengine mengi ambayo ninaamini msomaji unayafahamu au umeshawahi kuombewa. Nisikilize nikwambie kama hayo maombi unayoombewa yangekuwa yanatokea, mfano unaambiwa pokea muujiza wa gari halafu gari inatokea from no where au ukienda nyumbani unaikuta gari imepark hujui ilikotoka haina mwenyewe basi huo ndo muujiza lakini ukichukua hela ukaenda mwenyewe kununua gari hapo kuna muujiza gani ndugu? Au unaombewa pokea muujiza wa kwenda ulaya halafu ghafla unajikuta uko ulaya hujui umefikaje huo nao ni muujiza. 

Kitu gani nataka ujifunze hapa? Uache kuishi maisha ya kimiujiza kwa sababu mambo hayajileti yenyewe yanasababishwa kutokea,utanielewa tu huko mbele! Angalia Biblia yako nikuonyeshe mifano michache kuhusu miujiza halafu tuendelee, kutoka  7:10-12 inasema,

10………Haruni akabwaga fimbo yake chini mbele ya farao,mbele ya watumishi wake,ikawa nyoka.
11Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi;na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo 
Kwa uganga wao. 12Wakabwaga kila mtu fimbo yake,nazo zikawa nyoka;lakini fimbo ya Haruni
Ikazimeza fimbo zao”.

Sikia! hata ungewaita wanasayansi hapo hakuna ambaye angekueleza ile fimbo ya musa na za wachawi ziligeuka vipi zikawa nyoka! Huo ulikuwa muujiza lakini nataka ujifunze mambo machache hapa, kwanza fahamu Mungu anatenda miujiza lakini pia kama hufahamu shetani naye anatenda miujiza! Umeona hapo fimbo ya Musa ilipotupwa chini iligeuka nyoka na wachawi wa farao wakatupa zao nazo zikawa nyoka lakini (naupenda sana huu mstari) fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zile za wachawi! Unajua maana yake? Ni hivi, kile kitendo cha fimbo ya Haruni kumeza fimbo za wachawi Mungu alikuwa anamaanisha kwamba yeye ni mkubwa kuliko shetani,alikuwa anamaanisha muujiza wake ni mkubwa na unadumu kuliko wa shetani! 

Ngoja niishie hapo Mungu akitoa nafasi nitakuja na somo linalohusiana na miujiza na Baraka maana hivi ni vitu vinavyowasumbua sana watu kiasi cha kuwafanya waishi maisha ya kutanga tanga kwa kuhama kanisa hili kwenda kanisa jingine. Sasa angalia maneno anayosema Mtume Petro wakati analiandikia kanisa waraka wake wa kwanza na ninachotaka uone hapo ni yale maneno anayosema “mkijitahidi kwa UPANDE WENU”!  Sijui kama umeshawahi kutafakari mstari huu kwa makini na ukangundua yaliyojificha hapo; Petro anaposema kwa upande wenu ina maanisha kuna sehemu yako wewe kufanya kwa upande wako na kama kuna upande wako kufanya kitu basi  pia kuna sehemu ya Mungu kufanya kwa upande wake na  ndio maana kichwa cha somo kinasema mambo hayajileti  yenyewe kwa sababu kuna kitu unatakiwa kufanya kwa upande wako ambapo ukikiunganisha na upande anaofanya Mungu unapata jibu lako! Ngoja twende na mifano, angalia yeremia  29:12 – 14 inasema hivi:-
12 Nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza.13 Nanyi mtanitafuta,na kuniona,mtakaponitafuta
Kwa moyo wenu wote.14 Nami nitaonekana,asema BWANA,nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa……………….”.

Kwa tafsiri rahisi ni kama Mungu anasema,kwa upande wenu mnachotakiwa kufanya ni kuniita,mnachotakiwa kufanya ni kuniomba na kwa upande wangu ninachotakiwa ni kuwasikiliza,na kujionyesha kwenu! Maana yake ni nini? Kama huiti Mungu hawezi kuitika! Ndiyo! Ataitikaje wakati hajaitwa? Mpendwa unakumbuka ule mstari ambao hata ukimuuliza mtu asiye na tabia ya kusoma biblia atakutajia mstari huo? Ni ule wa mathayo 7:7, hebu uangalie kwa namna hii nilivyofanya ili kukurahisishia kuelewa!
Upande wako kufanya kitu                                                  upande wa Mungu kufanya kitu
Ombeni nanyi (kuomba)                                                       mtapewa  (kukupa unachoomba)
Tafuteni nanyi (kutafuta)                                                      mtaona (kukuonyesha unachotafuta)
Bisheni nanyi   (kubisha/kupiga hodi)                                 mtafunguliwa (kukufungulia malango)

Kumbuka mambo hayajileti yenyewe bali yanasababishwa kutokea na kwasababu hiyo hauwezi kufanikiwa katika jambo lolote kama utakuwa ni mtu wa kukaa na kusubiri Mungu afanye kitu na hata kama Mungu akifanya kitu amefanya kwa upande wake kama wewe hujafanya  kwa upande wako hauwezi kupata matokeo! Angalia mfano huu nikuonyeshe kitu, fungua Yohana 9:6-7 inasema hivi,
6 Alipokwisha kusema hayo,alitema mate chini,akafanya tope kwa yale mate.
Akampaka kipofu tope za macho,7 akamwambia,nenda kanawe katika birika ya Siloamu,
(maana yake aliyetumwa).Basi akaenda na kunawa;akarudi anaona”.

Hii ni habari ya mtu mmoja aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa  na kwa bahati akakutana na Yesu lakini katika kuponywa kwake kuna kitu alitakiwa afanye kwa upande wake ili kukamilisha uponyaji wake na kilikuwa ni kwenda kunawa kwenye birika ya siloamu na biblia inasema akaenda na kunawa akarudi anaona! Kama yule kipofu angeamua kudharau akapitiliza na kuendelea na mambo yake mengine asiende kunawa ninakwambia angebaki kipofu hivyo hivyo lakini si kwa sababu Mungu hakufanya kitu,hapana, Mungu alishafanya kwa upande wake na ilibaki sehemu yake yule kipofu kufanaya ili kukamilisha uponyaji wake!
Okey! Angalia mfano wa mtu mmoja aliyekuwa na ukoma jina lake Naamani, huyu alimwendea mtumishi wa Mungu Elisha baada ya kusikia kuwa anaweza kumponya. Alipofika kwa Elisha,alitumiwa ujumbe wa mtu kumwambia kuwa aende katika mto Yordani akajichovye mara saba na ngozi ya mwili wake itarudi kuwa kawaida kabisa. 

Naamani aliposikia hivyo alikasirika na kusema,”Tazama,nilidhania,bila shaka atatoka kwangu, na kusimama na kuomba kwa jina la BWANA,Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali penye ugonjwa na kuniponya mimi mwenye ukoma. Je abana na farpari,mito ya Dameski si bora kuliko mito yote ya Israel? Siwezi kujiosha ndani yake na kuwa safi? Akageuka akaondoka kwa hasira”.
(soma habari hii katika kitabu cha 2wafalme 5:9-14) Haya ndiyo mwazo waliyonayo watu wengi sana wanapokwenda kanisani au kwenye semina na mikutano ya neno la Mungu au wanapofanyiwa maombezi. Unakuta mtu haamini mpaka awekewe mikono na mtumishi, lakini nataka nikwambie kitu kimoja ambacho watu wengi wamekuwa wanakosea ambacho ni kutokuafuata maagizo wanayopewa na watumishi au kutofuata vile neno linavyosema. Sikia! Kama umeambiwa kanawe katika birika ya siloamu nenda kanawe! Kama umeambiwa kajioshe kwenye mto yordani, nenda kajioshe! Kama umeambiwa endelea mbele hata kama mbele yako kuna bahari, wewe endelea mbele!!! JUST DO IT! Upande wa Naamani ulikuwa ni kujiosha kwenye mto Yordani tu na hakuna kingine na ndio maana wale watumishi walimwambia maneno haya,”Baba yangu kama yule nabii angelikuambia kutenda jambo kubwa,usingalilitenda? Je si zaidi basi akikuambia,Jioshe uwe safi?” nachotaka kukuambia hapa ni wewe kufuata maagizo ya neno la Mungu linavyosema. Kwa hiyo nabii Elisha alifanya kwa upande wake na ulibakia upande wa muhitaji ambaye ni naamani, na lipokubalikufuata maagizo alipona kabisa!(haleluya!) Petro anasema mkijitahidi kwa upande wenu, (kumbuka hilo). 

SHANGILIENI WAFANYA HUDUMA KUBWA HOSPITALI YA KCMC MOSHI

Kwaya kongwe nchini ya Tumaini Shangilieni kutoka kanisa la Mtakatifu James jijini Arusha, imefanya uinjilisti mkubwa usiku wa kuamkia jumamosi iliyopita katika hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro, waimbaji hao walitoa huduma kwa kugawa vitu mbalimbali kwa wagonjwa pamoja na kuwafariji na kuwaombea kwamba Mungu awaponye katika magumu wanayopitia.

Kati ya matukio ambayo yaliwasisimua waimbaji hao ni kumuona kijana mdogo ambaye amelazwa hospitalini hapo kwa takribani mwaka mzima baada ya kuungua vibaya kwa moto. Baada ya huduma hiyo hospitalini waimbaji hao waliungana na waimbaji wengine walioalikwa kwa tukio la mkesha wa uimbaji ulioenda sambamba na mdahalo kuhusu tasnia ya uimbaji uliofanyika katika kanisa la chuo, ambapo waimbaji waalikwa kama Abednego Hango wa New life band, Jackson Benty, mchungaji Mgondo wa Zion temple wote wa Arusha walihudhuria pamoja na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.

Baadhi ya waimbaji wa Tumaini wakiwa wamewasili hospitalini hapo tayari kwa huduma.






Walihitimisha kwa maombi mazito.
Kati ya majembe ya Tumaini choir, Wilson na uncle wake Emmanuel Mtangoo ambaye ni mwenyekiti wa kwaya wakikung'uta magitaa.
Tumaini wakimsifu Mungu. 

Emanuel Mtangoo mwenyekiti wa kwaya akionyesha mfano wa kucheza kwa Mungu wake.
Pastor Mngodo wa Zion Temple akizungumza jambo.

Abednego Hango wa Newlife Band akitoa mada kwenye mkesha huo.

Monday, 20 May 2013

MUULIZE via GK : SARAH K HAJABAKIZA KITU KATIKA MASWALI YAKO

Hujambo msomaji wetu wa Gospel Kitaa, karibu katika kipengele chetu cha "MUULIZE via GK" ambacho kinakujia kila siku za jumamosi ndani ya GK kinachokupa fursa ya kumuuliza muimbaji ama mtumishi yeyote wa Mungu swali moja kwa moja kupitia ukurasa wa Gospel Kitaa, na kwa kushirikiana na Gospel Celebration, utayapata majibu yako kwenye kipindi. Siku ya jumamosi mama mchungaji Sarah K kutoka nchini Kenya amejibu maswali ambayo umemuuliza kupitia ukurasa wetu wa facebook. Karibu usikilize sauti za majadiliano, na pia ujisomee mwenyewe hapo chini mazungumzo yote.



                        

  • Martha Richardy Niko Mza, huyu dada huwa namkubali sana hasa wimbo wake wa 'Liseme' na 'Mnyunyizi wng' kwa kweli huwa haipiti siku sijazisikiliza. Nampongeza na Mungu azidi kumtumia. Swali langu ni....1. Ameolewa na ana watoto wangapi. 2. Ni kabila gani


Sarah K : haha(kicheko) aah nimeolewa nina watoto watatu na kabila mimi ni Mkenya, kuna mengi sasa ambayo hayahesabiki ndio maana mimi kujiita Mkenya.





Sarah K : ooh okay sielewi ni kwanini kwasababu nina msambazaji anayesamabaza Tanzania anajiita muhubiri yuko na maduka Dar es salaam naa nafikiria Moshi ama Arusha ana maduka mawili hapo kwahivyoo sijui ni kwanini lakini kuna watu wengine wengi ambaoo wanachukua kusambaza maeneo mbalimbali ya Tanzania, naelewa kwamba Tanzania ni kubwa kwahivyoo sijui anayeuliza swali yupo upande upi wa Tanzania lakini naelewa wengi wao huja Dar es salaam ama Arusha au Moshi halafu wanazichukua ndipo wanazipeleka.





Sarah K : eeh nimeolewa na nina watoto watatu




Sarah K : Amen, Mungu ambariki pia.


  • Steven Licheula WA KIBAHA. DADA SARH,NYIMBO ZAKO ZINAGUSA WENGI.ILI KUNA MAMA NAOMI WA MWANAGATI HUYU MAMA AKISIKIA WIMBO WA LISEME HULIA JE UNAMSHAULI NINI HUYU MAMA?


Sarah K : Nimeshaona nimeshaona hivyo kuna hata nikiwa mara nyingi nikienda kuu kwenye kanisa ambako ninakwenda kuhudumu ninajikutaga hata mimi mwenyewe nalia kanisa pia hata watu wengi wanalia kwasababu una mguso wake ambao kwamba pengine kuna mambo ulishafikia hatua pengine umekata tamaa yaani ile basi kama vile mtu Mungu amemsahau, ama pengine ni kwenye mpango wa Mungu siku nyingine nikapata haya au pengine Mungu alipanga basi mimi nitakaa hivyohivyo, lakini ukishasikia maeneno hayo kwamba anasema hakuna jambo asiloliweza mara nyingi nisisi yeye anatusubiri sisi tumpe mahitaji yetu ni kama kwajinsi vile mtoto mimi kama mzazi kuna mambo mengine ninajua mtoto anahitaji lakini mengi ni yale yatakuja aniambie mama nahitaji hivi mama nasikia njaa kwahivyo hata kukiwa na chakula sitashughulika asiponiambia....... kwahivyo Mungu anatuambia tutu tusishughulike sisi wenyewe tusijetukafichaficha ama tukajifanya hatutaki kuyataja, tumwambie waziwazi ndivyo ninavyoomba yani nikulisema linalonitatiza, ugonjwa huu nimekaa nao kwa muda mreeefu sasa Mungu ninausema kwako uniponye, sasa wengine wakisikia sasa nimekaa na hili jambo wakati huu wote na Mungu anasema kwasababu hii ni kama sauti ya Mungu mwenyewe anasema ni lipi hilo yeye asiloliweza. Hivo mimi namshauri tu kwamba aendelee kumtazamia Mungu naaa vile unavyosikia moyoni mwako kulia alie kwasababu anamlilia kwa hali ya kumshukuru Mungu na kujua kwamba atatenda yote maana neno lake nila ukweli naa amina


  • Angel Hosiana Niko ubungo, kwa kweli na mpenda sana huyu dada mungu ambariki sana.. Ningependa kujua ana 
    1:albam ngapi na alianza lini huduma ya uimbaji
    2:yeye ni kabila gani?


Sarah K : aahmmh huduma ya uimbaji niliianza kitambo maana niliianza kanda yangu ya kwanza kurekodi nilirekodi mwaka 1991 lakini nilianza kuimba kwa kama vile nilivyosema hapo awali Kenya kuna makabila mengi kwahivyo kwa kabila moja ambalo langu ni la tunaita mother tongue nilianza kuimba kwa kilugha kwanza kwa album kama tatu hivi kwahivyo nina album kama tatu za kilugha halafu mwaka wa 2000 ndio nilitoa album ya kwanza iliyokuwa inaitwa aah Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni hawatatikisika milele ina Wamtumainio Bwana, Mwimbieni Bwana nyimbo kama hizo. Halafu mwaka 2003 ndio nikatoa wimbo unai title yake ni Milele Daima unawimbo unasema Nasema Asante, hivyo ukijumlisha zote za kiswahili sasa ambazo eeh ni za Kiswahili na English eeh kama Wamtumainio, Milele daima, Adonai, Testimony, mmmh nanyingine na sasa Liseme na nimetoa album nyingine mpya ya sita ambayo ni mpya sana pengine ina siku kadhaa kwahivyo za Kiswahili ni sita na za kilugha kama tatu hivi.




Sarah K : Amen.



  • Rehema Mmbando wa dar. mungu akubariki sana dada sara kwa uduma yako .swali langu huwa unasaidiaje wale waimbaji wachaga yani anderground ? na umeanza uduma yako ya uimbaji lini? karibu tz


Sarah K : aah nawasaidia kwamba wasife moyo halafu aahmmh (anajaribu kutafsiri neno kwa kiswahili) yaani wafuatilie ndoto zao na maono yao kwasababu kuna mambo mengi ambayo yanaweza kuja hata katika uimbaji yanakupotosha, yanaweza kukwambia kwamba umefika kumbe bado hujafika kwa mfano nitakutolea mifano mbili hili linaweza kuzungumziwa kwa urefu sana aaah katika uimbaji inaweza ikaja ukiwa mchanga halafu Mungu akakupa kibali sana ukaa ukawa na kibali mbele ya watu zaidi wimbo wako ukapendwa na ukauzwa sana sasa hapo kikwazo kimoja kinaweza kukufanya ukarudi nyuma ni zile hela utakazozipata kutoka kwenye uimbaji ule zinaweza kukutikisa ukarudi nyuma ukakosa kufuatilia yale maono yako uliyokuwa ama ahadi ulizweka mbele za Mungu ya kwamba Mungu, unajua kuna ahadi zile uliweka wakati uko chini kabisa ukamwambia Mungu utakaponivusha, utakaponibariki nitafanya hivyo kwahivyo unajikuta umesahau. la pili ni ile umaarufu wakati wimbo wako umehit ukajulikana sana kuna ile fame unaipata kila mtu anakuita Sarah K Sarah K kila mtu anaongea juu yako radio stations zote zinakutaja nanini kwahiyo hiyo fame ikishaingia ndani yako na uikubali kwamba wewe uko maarufu ama uko mtu maarufu kama vile tunavyosema hapo sasa ndipo kiburi kitaanza kujiinua na utaanza badala ya kuwa watu wanakuombea, uwe mnyenyekevu tu daima na umshukuru Mungu juu ya kwamba wewe si kwamba umefanya kitu kizuri sana ni ile neema ya Mungu tu halafu unyenyekee zaidi unaanza kujiinua na unaona kwamba watu wamekuwa wasumbufu hiyo basi inakurudisha nyuma cha kufanya yale maono uliyokuwa nayo wakati uko chini kabisa wakati unamuomba Mungu utayafikia kwasababu kuna mambo mawili kuna hela na kuna kiburi, kwahiyo kuna mambo mengi naweza ongea lakini kwanza ngoja niachie kwasababu ya muda.




Sarah K : Ameen, aah kama vile nilivyosema nilianza kuimba 1991 miaka ishirini na mbili na tatu hivi kwahiyo hapo nilianza kuimba nikiwa na umri wa miaka 21.


  • Konoise Kyejo Wa kitunda ubarikiwe kwa huduma hiyo nina maswali3 kwa kifupi 1.unaweza kutoa huduma ukialikwa vijijini au nje ya mji? 2Tumekuwa tukitumia nyimbo zako sn kama Ringtune je unalipwa? 3 Je? Unaabudu kanisa g


Sarah K : Okay nitaanza na la tatu naabudu kanisa la Kianglikana mimi ni mshirika wa wa wa wa dhehebu la Kianglikana maana mume wangu ni mchungaji katika Kiangliakana kwahiyo tuna hudumu pamoja la pili alikuwa anauliza kama ninalipwa kwenye ringtone hapa Kenya tuna nimesha saini mkataba kwahiyo kama ni za Kenya nalipwa kwa Tanzania sijui maana sijui hata kama wako nazo maana sijawahi kuwa katika kampani yoyote hivyo ina maana kama Tanzania wanauza basi sijawahi lipwa, la kwanza niko tayari kwenda lakini huwa nina kitu kimoja ambacho naambia watu kwamba ujue wakati unamwalika mtu kutoka mbali kila kitu kina garama yake hakuna kitu duniani ambacho hakina gharama yake kwahivyo kama unamwalika mwimbaji kama sasa Sarah K unamwalika kutoka Kenya kuja huku ujue kwamba kuna gharama zake zaa zaa zakuja naa utamlipa kama tu unavyomwalika mgeni ya kwamba basi utampikia na utampa mahali pa kulala pazuri vitu kama hivyo ndio unamwambia kwamba kila kitu unataka kukitenda kizuri kinagharama yake hivyo kama unaona kwamba huwezi hujafika Mungu hajakushuhudia hujafika kulipa hiyo gharama mwite mwimbaji aliyekaribu na wewe kwasababu kama ni huduma ya Mungu unataka ili watu wabarikiwe mwite muhuduma ambaye yupo karibu nawewe utaweza kulipa gharama hiyo mpaka Mungu atakapokusaidia uendelee kumuona na kumwamini akupe njia ya kukupa ili uweze kugharamia yule unayemtaka wa mbali ili nayeye asijeakaja akaumia roho akaona ametoka mbali halafu akawa ameumia kwasababu yote ni kuhudumu tunahudumu kama unajua waimbaji hatuna hatuna njia yoyote unayofanya ya kwamba naweza sema nitajilipia ndege au basi najilipia maladhi kwasababu nimealikwa... kwa hivyo kazi yangu ambayo Mungu amenipa ni hii kwahivyo wanaonigharamia au watu wote wanaonialika ndio wanaotakiwa kunifanyia haya yote hivyo ndio tu ninataka kabla mtu ajaniita huwa ninamshauri nanina mwambia hivyo isije ikawa mzigo sana kwayeye kuniita mimi.




Sarah K : Amen


  • Maria Julius wa mbagala mission shalom mpendwa sio siri navutiwa na kazi yako dada mungu akubaliki ningependa kujua nini matarajio yako ya baadae.ubarikiwe sana


Sarah K : aaahmm swali ni ngumu iyo matarajio yangu ya baadaye ni kwamba aah kama jinsi ni kitu cha kwanza ni Mungu lakini la kwanza la muhimu sana kwangu ni kwamba waimbaji tume tumekuwa na tabia ya kwamba kumekuwa na tabia katika uimbaji na niliikuta wakati mimi nilianza, mwimbaji anaanza kipindi fulani halafu anaisha sema anasikia kuna mwimbaji alikuwa fulani fulani lakini siku hizi hasikiki hata kidogo na yupo tu bado yupo anaendelea anaishi lakini ni kama haimbi tena hata kama akiimba haijulikani yuko vipi au unasikia aliimba vizuri vizuri zile nyimbo za kwanza lakini hizi za mwisho mwisho hazieleweki. Ombi langu ni kwamba namwamini Mungu nitaendelea katika huduma yangu ya uimbaji hata kama nitakuwa na miaka 90 hata kama nitakuwa na miaka 80 niendelee kumwimbia Mungu kwanjia ya uimbaji na hayo na hiyo italetwa kwa kuwa mnyenyekevu na mtiifu mbele za Mungu sio mbele za watu tu, katika utunzi wangu nina muhusisha Mungu zaidi ya mimi mwenyewe ninavyojiona kwasababu nina album 10 ama 9 yani nina ujuzi kabisa wa utunzi kwahivyo sihitaji Roho mtakatifu simuhitaji Mungu aah nasasa hiyo ndio sali yangu ndio maono yangu kwamba sitaacha kuimba sifa zaidi Mungu anisaidie nisijulikane tu sasa hivi, hata nitakapofikisha miaka 70 yani nitaendelea nanitabariki watu nitakuwa ninawajenga watu mioyo yao nitakuwa nawainua watu mioyo yao ambao ni wadhaifu kwenye maeneo ambayo Roho Mtakatifu ananipa watasikia wameinuka na kuwa na matarajio kwamba Mungu yupo na ataendelea kuwatendea makuu ni mengi tu wacha niachilie hapo kwanza.


  • Ricious John Jamani Mungu akubariki kwa huduma yako! Na barikiwa sana na nyimbo zako! Hv iyo K' kirefu chake ni nn! BARIKIWAAAAAAH!


Sarah K : hahaha (kicheko) Amen, kirefu chake ni Kiarie yaani Sarah Kiarie ndio nikaichia tu kwa K


  • Flazia Isack Nimekuwa nikisikia kuwa waimbaji wengi hasa in east africa wamekuwa wakifanya kazi zao Tz so as to earn more na sio kutimiza kusudi la Mungu, what about you on your side? tc frazia from Ardhi university....


Sarah K : Okay sasa well naweza semaje haya mambo mawili hayastahili kuachana maana kusikika kutakusaidia maana watu wengi watakusikia na wataweza kujua lile jambo Mungu ameweka ndani ya moyo wako ili wanaposikia liwajenge maana Mungu akiweka jambo moyoni mwako halafu lisisikike lisijulikane basi litakuwa lipo tu liko tu ndani yako hakuna mtu mwingine anayefaidika kwalo hivo ni vizuri usikike na ujulikane ndio Mungu akusaidie yaani usikike na ujulikane ili jambo ambalo ameweka ule mzigo ambao ameweka ndani yako lile neno la Mungu ambalo ameweka ndani yako lile neno la Mungu ameliweka ndani yako ili uweze kulitoa kwa njia ya Roho Mtakatifu atakavyokusaidia liweze kusaidia watu liweze kuponya watu liweze kuinua watu kwahivo hayo mambo mawili hayastahili kuachana haistahili kuona wewe unaimba ili ujulikane tu peke yake yaani inastahili kama wewe .. ninakumbuka siku moja nili nili nilikuwa nawaambia waimbaji nilisema kuwa hebu tuache maombi haya mafupi ya kusema kuwa Mungu mimi naimba kwa utukufu wako tu tunaachia hapo ukiimba kwa utukufu tu wa Mungu unaishia hapo anasema liseme na umelisema tu hilo basi itaachilia hapo kwa utukufu wa Mungu pale litanyamaza tu hivyo hutakuja kujulikana hata siku moja kwasababu umeimba tu ni kwa utukufu wa Mungu ni hivyo sema endelea kutaja sema ya kwamba Mungu ningependa niimbe kwaajili yako kwa utukufu wa jina lako na unisaidie unipatie fedha ili uimbaji hii kanda ili watu wengi waijue ili isikike na watu wengi waweze kusaidika wengi waweze kupona wengi waweze kuinuka wengi hivyo namaanisha kwamba haya mambo mawili hayastahili kuachana yanastahili kwenda sambamba

  • Dotto RK Kutoka Kigamboni bwana yesu asifiwe dada,napenda nyimbo zako kama vile LISEME na MNYUNYIZI zinanibariki sana nataka kujua alikua ktk mazingira gani wakati akiandika hizo nyimbo,pia vipi mwaka huu mbona kimya.BARIKIWENI WOTE HAPO

Sarah K : Ameen, sasa kwenye mazingira ya liseme na mnyunyizi, inaweza kuwa mambo marefu ambayo ntaongea lakini nitasema ya kwamba ... ni ile tu hali ya kuwa unaongea na Mungu halafu na ile hali ya kungojea majibu na kumsikiliza Mungu anakujibu, katika hali yangu ya maombi yaani nilikuwa naomba, ananijibu kwa liseme ikaja kulingana na maandiko yake. Sitaongea sana kuhusu hayo kutokana na muda, lakini nieme kuwa mwaka huu sijanyamaza, kama vile nilisema awali, nimesharelease another album lakini iko kwa audio peke yake VCD bado, imekuwa, I think this is the fourth or the third day, ni siku ya tatu nimeanza kuipeleka kwenye maduka kwa hivyo ipo, itawafikia